Trofimo wa Efeso

Trofimo wa Efeso

Trofimo wa Efeso (kwa Kigiriki: Τρόφιμος ὁ Ἐφέσιος, Tróphimos ho Ephésios; alifariki Sinnada, Frigia, leo nchini Uturuki[1]) alikuwa Mkristo kutoka mji huo wa Asia Ndogo (Mdo 20:4) aliyeongozana na Mtume Paulo na wenzake wengine katika sehemu ya safari yake ya tatu ya kimisionari hadi Yerusalemu[2].

Kwa kuwa alikuwa mtu wa mataifa (Mdo 21), Wayahudi walidhani kwamba Paulo alimuingiza mpaka ndani kabisa ya Hekalu, sehemu ambayo ilikuwa kwa taifa lao tu (Mdo 21:28). Ndiyo sababu ya jaribio la kumuua Paulo lililoishia katika miaka zaidi ya 4 ya kifungo kati ya Kaisarea Baharini na Roma (58-63).

Baada ya kurudishiwa uhuru, Paulo alimuandikia Timotheo kwamba alimuacha Trofimo huko Mileto kwa sababu ya ugonjwa.[3] Habari hiyo inahusu safari nyingine iliyofuata.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Septemba[4].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/70760
  2. "www.Bibler.org - Dictionary - Trophimus". 2012-07-26.
  3. 2Tim 4:20
  4. Martyrologium Romanum

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search